×

Rashford Arejea Manchester United Apewa Jezi namba 14

Staa wa Manchester United Marcus Rashford amerudi katika kambi ya maandalizi ya  baada ya kumaliza mkopo wa msimu mmoja na mabingwa wa Hispania FC Barcelona, nyota huyo amejiunga na kikosi kinachoendelea na maandalizi huko Ireland chini ya kocha Michael Carrick.

United imeamua kubaki na Rashford na kumrejesha kwenye mipango ya timu, na taarifa zinaeleza kuwa atavaa jezi ya namba 14 ishara kuwa klabu ina mpango wa kumbakisha Old Trafford badala ya kumuuzia au kumuachia mkopo tena.

Rashford ameungana na pamoja na wachezaji wengine waliokuwa likizo baada ya Kombe la Dunia kama Mathius Cunha, Matthijs de Ligt, Kobbie Mainoo na kipa Simon Lammens.

Akiwa ana Barcelona, Rashford alicheza michezo 49 katika michuano yote na  kufunga magoli 14 na asisti 11 na kufanikiwa  kubeba mataji mawili La Liga na Supercopa de España.

 

Leave a Comment