
Leo hii unaweza ukatengeneza pesa ndefu kwa kusuka jamvi lako la ushindi na Meridianbet. Timu kibao zenye Odds kubwa zipo kwaajili yako, ingia na usuke jamvi siku ya leo.
Kule Saudi Arabia ligi kuu itaendelea yaani SAUDI PRO LEAGUE ambapo Al-Fahya atamenyana dhidi ya dhidi ya Al Hilal ambao walianza vyema kampeni yao ya msimu huu kwa kupata ushindi kwenye mechi yao ya kwanza wakati wenyeji wao wakipoteza.
Kwa upande wa Al Hilal wanataka kupambania taji la ligi msimu huu baada ya msimu uliopita kukosa taji hilo mbele ya Al Nassr, hivyo hii ni mechi ambayo ina umuhimu mkubwa sana kwao kwani Waswahili husema biashara asubuhi, na jioni ni mahesabu.
Al Fahya ni timu ya daraja la kati ambayo pia kule kwa wakali wa ubashiri Meridianbet hapewi nafasi kubwa ya kushinda mechi hii kutokana na ubora wa timu ambayo anakutana nayo yenye wachezaji wenye ubora mkubwa akiwemo Karim Benzema.
Mechi hii pia imepewa machaguo zaidi ya 1000 ambayo mteja anaweza akataytumia kwa kufanya ubashiri na kuondoka na ushindi mkubwa, kama vile kona, faulo, 2UP, na mengine ambayo mteja anataka.
Hii ni mechi ambayo mwenyeji anahitaji kulipa kisasi kwa hali na mali au kumaliza uteja mbele ya timu hii kwani kwenye mechi zao 5 za misho kukutana Al Hilal ameondoka na ushindi mechi zote. Je wewe nafasi ya ushindi unaiweka wapi?. Suka jamvi hapa.
Mkwanja upo kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.
Pia NBC PREMIER LEAGUE kitapigika haswa Yanga atakuwa nyumbani kumenyana dhidi ya Coastal Union. Baada ya kushinda kule ugenini sasa Yanga watakuwa wakisaka ushindi wa pili, huku Wagosi wa Kaya wao wakipoteza mechi ya kwanza ya ligi wakiwa nyumbani kwao. Vijana wa Manqoba wao ni mabingwa watetezi wa ligi mara tano mfululizo huku wakihitaji ushindi kuendelea kutetea taji lao.
Mabingwa hawa watetezi kuelekea msimu huu mpya wa ligi waliweza kufanya usajili mkubwa wa wachezaji wenye uwezo mkubwa akiwemo Peter Shalulile, Zakuone, Toure na wengine wengi ambao kwa pamoja wataisaidia klabu hiyo kufanya vyema. Lakini wamemrejesha Aziz Ki ambaye huenda akaonekana kwenye mchezo huu wa leo.
Coastal wao ni timu ambayo msimu uliopita halikuwa na msimu mzuri kwani ilinusurika kucheza play offs, hivyo wanaweza wakaingia kwenye mchezo huu kwenda kujilinda zaidi kuliko kushambulia. Nani kuondoka na ushindi leo?. Beti hapa.
Takwimu zinaonesha kuwa mechi tano za misho kukutana timu hizi mbili kwenye ligi, Yanga wameondoka na ushindi mechi zote, na mara ya mwisho Coastal kupata ushindi mbele ya vijana hawa wa Jangwani ilikuwa ni 2021. Jisajili hapa.