×

Rais Samia Awatakia Waislamu Kheri katika Maadhimisho ya Maulid

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewatakia Waislamu na Watanzania wote kheri na baraka katika Maadhimisho ya Sikukuu ya Maulid.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Rais Samia amesema Maulid inapaswa kuwa ukumbusho wa kuendelea kuishi kwa upendo, huruma, uvumilivu na kuwajali wengine katika jamii.

Amesisitiza umuhimu wa Watanzania kusherehekea Maulid kwa amani na furaha, huku wakidumisha umoja na mshikamano unaoendelea kuijenga Tanzania.

Rais Samia pia amemuomba Mwenyezi Mungu kuendelea kuibariki Tanzania, kuitunza katika amani na utulivu, pamoja na kuwawezesha wananchi kuijenga nchi kwa maendeleo na ustawi wa wote.

“Tusherehekee kwa amani na furaha huku tukidumisha umoja na mshikamano wetu. Mwenyezi Mungu Mtukufu aendelee kuibariki nchi yetu, kuitunza katika amani na utulivu, na kutuwezesha kuijenga kwa maendeleo na ustawi wa wote,” amesema Rais Samia.

Leave a Comment