
Muigizaji wa filamu na mwanamitindo Serayah ametangaza kuachana na mchumba wake, rapa Joey Bada$$, huku akidai kuwa msanii huyo alikuwa akimsaliti mara kwa mara katika kipindi cha uhusiano wao.
Serayah, anayefahamika pia kwa nafasi yake katika tamthilia Empire, amedai kuwa usaliti huo uliendelea kujitokeza katika vipindi mbalimbali vya uhusiano wao, ikiwemo wakati alipokuwa akipitia changamoto za maisha.
Wawili hao walikutana mwaka 2021 kupitia sherehe ya siku ya kuzaliwa ya rafiki yao na baadaye wakaanza uhusiano wa kimapenzi.

Uhusiano wao uliendelea kwa miaka kadhaa, ambapo mwaka 2025 walipata mtoto pamoja na kutangaza uchumba wao.
Hata hivyo, uhusiano huo umefikia mwisho huku Serayah akieleza madai ya kutoridhishwa na mwenendo wa Joey Bada$$ katika kipindi walichokuwa pamoja.
Taarifa kuhusu kuvunjika kwa uhusiano wao zimeibua hisia mbalimbali miongoni mwa mashabiki, hasa kutokana na wawili hao kuwa wamekuwa wakionekana pamoja hadharani na kushirikiana katika malezi ya mtoto wao.
Hadi sasa, Joey Bada$$ hajatoa maelezo ya kina kuhusu madai yaliyotolewa na Serayah.
