Baadhi ya mashabiki wa Simba wameonekana kutoridhishwa na kiwango cha mshambuliaji wa klabu hiyo, Ibrahim Doumbia, licha ya timu hiyo kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Coastal Union FC.
Mchezo huo umechezwa katika Uwanja wa Isamuyo, ambapo shabiki wa Simba, wametoa maoni yao kuhusu kiwango cha Doumbia wakati akizungumza na mtangazaji wetu Official Diana, mara baada ya mchezo kumalizika.