×

Mafuriko Yaua Watu 100 Nepal, Zaidi ya 1500 Hawajulikani Walipo

 

Idadi ya watu waliopoteza maisha kutokana na mafuriko makubwa yaliotokea nchini Nepal imefikia 165, huku wengine 1,300 bado hawajulikani walipo,  mafuriko hayo yamesababisha uharibifu mkubwa katika maeneo ya mpakani mwa Nepal na China.

Mafuriko hayo yalitokea Jumatano, Agosti 26, yakisababisha vifo, uharibifu wa miundombinu na kutoweka kwa mamia ya watu katika maeneo yaliyoathirika. Vifo vingine vitatu pia vimeripotiwa upande wa Tibet, China.

Janga hilo lilisababishwa na kuporomoka kwa barafu kubwa kutoka kwenye milima ya Himalaya, na kusababisha maji mengi, vipande vya barafu, mawe na matope kusukumwa kwa nguvu kuelekea kwenye mfumo wa mito na kuvamia maeneo ya makazi.

Utafiti wa Jiolojia wa Marekani (USGS) umeeleza kuwa ishara ya awali ya mtikisiko iliyodhaniwa kuwa ni tetemeko la ardhi haikusababishwa na tetemeko, bali ilitokana na kuporomoka kwa barafu pamoja na mabaki ya miamba na udongo.

Mafuriko hayo yamesababisha uharibifu mkubwa wa nyumba, barabara na madaraja, huku baadhi ya maeneo yaliyoathirika yakibaki kuwa magumu kufikika kutokana na miundombinu kuharibiwa.

 

Timu za uokoaji zimeendelea na operesheni za kuwatafuta manusura na watu waliopotea kwa kutumia helikopta, ndege zisizo na rubani (drones), mbwa maalumu wa utafutaji na vifaa vingine vya dharura.

Mamlaka zimeripoti kuwa  madaraja 19 na takribani kilomita 40 za barabara zimesombwa na maji nchini Nepal, hali inayozidi kufanya shughuli za uokoaji kuwa ngumu.

Waokoaji wanaendelea na juhudi za utafutaji katika maeneo mbalimbali, huku mamlaka zikionya kuwa idadi ya waliofariki inaweza kuongezeka kutokana na uwepo wa watu wengi ambao bado hawajulikani walipo.

Leave a Comment