×

Polisi Arusha Wamkamata Godlisten Malisa, Aachiwa Kwa Dhamana

Jeshi la Polisi Mkoani Arusha limemkamata Godlisten Elisante Malisa pamoja na mwenzake kwa tuhuma za jinai zilizokuwa zikichunguzwa dhidi yao.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi, Malisa na mwenzake walikamatwa jana, Agosti 31, 2026, majira ya usiku mkoani Arusha.

Baada ya kukamatwa, wawili hao walifanyiwa mahojiano kuhusiana na tuhuma zilizokuwa zikichunguzwa dhidi yao.

Jeshi la Polisi limeeleza kuwa baada ya mahojiano, Malisa na mwenzake waliachiwa kwa dhamana, huku wakisubiri kukamilishwa kwa taratibu nyingine za kisheria.

Taarifa hiyo haijaeleza kwa undani aina ya kosa la jinai linalochunguzwa wala hatua nyingine zitakazochukuliwa dhidi yao, zaidi ya kueleza kuwa taratibu za kisheria zinaendelea.

 

Leave a Comment