Kesi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, imeahirishwa hadi kesho Septemba 2, 2026, huku Katibu Mkuu wa chama hicho, John Mnyika, akitarajiwa kuendelea kujibu maswali kutoka upande wa Serikali.
Katika hatua za mwisho za mwenendo wa kesi leo, Mnyika alikabiliwa na maswali kuhusu uelewa wake wa sheria, majukumu yake kama Katibu Mkuu wa CHADEMA, pamoja na kauli na msimamo wa chama kuhusu uchaguzi na vurugu.
Wakili wa Serikali, Nzengeli, alimuuliza Mnyika kama yeye ni mtaalamu wa sheria, ambapo alijibu kuwa si mtaalamu wa sheria.
Mnyika pia alikataa kuwa hana uwezo wowote wa kuchambua nyaraka, akisema anaweza kuchambua mambo kwa uelewa wake, ingawa baadaye alikiri kuwa hana utaalamu wa kisheria.

MNYIKA AULIZWA KUHUSU DEMOKRASIA
Katika dodoso hilo, Mnyika alieleza kuwa endapo mtu anaamini uchaguzi ni wa haki na uhuru, lakini CHADEMA ina msimamo tofauti, mtu huyo anaweza kutokubaliana na msimamo wa chama.
Alisema kutokubaliana na msimamo wa CHADEMA ni suala la maoni ya mtu binafsi.
Wakili Job Mrema naye aliendelea kumuuliza Mnyika maswali akitumia Kamusi Kuu ya Kiswahili, Toleo la Tatu la mwaka 2022, katika kutafuta maana ya baadhi ya maneno yaliyotumika kwenye ushahidi.
Mnyika alithibitisha kuwa kamusi hiyo ni rasmi, ingawa si nakala pekee inayoweza kutumika kutoa tafsiri ya Kiswahili.
Mrema alimuuliza Mnyika kuhusu majukumu yake kama Katibu Mkuu wa CHADEMA.
Mnyika alisema jukumu lake ni kusimamia shughuli zote za kila siku za chama.
Alipoulizwa kama ameshindwa kutaja majukumu yake katika baadhi ya maswali yaliyoulizwa awali, Mnyika alikanusha na kusema amejibu maswali mengi, isipokuwa machache ambayo yalihitaji uelewa zaidi.
Mnyika pia alikanusha madai kwamba nafasi yake ya Katibu Mkuu imekuwa ya kusaidiwa au kwamba amekuwa akibebwa na Mwenyekiti wa CHADEMA.
MNYIKA AULIZWA KUHUSU “FUJO”
Katika sehemu nyingine ya dodoso, Mrema alimuuliza Mnyika maana ya neno “fujo.”
Mnyika awali alijibu kwa kusema, “Fujo ni fujo,” lakini baada ya kuombwa kueleza maana hiyo kwa mujibu wa kamusi aliyokuwa nayo, alisema fujo ni hali ya kutokuwepo kwa utaratibu mzuri au mpango, pamoja na hali ya ghasia na machafuko.
Wakili Mrema alimuuliza Mnyika kama kauli iliyotolewa na Lissu Aprili 3, 2025 kwamba “ataleta fujo” na “atakinukisha” ilikuwa ni fujo yenyewe.
Kutokana na muda, upande wa Serikali uliomba suala hilo liendelee kesho, na Jaji akaelekeza kuwa swali hilo litashikiliwa kwa ajili ya kuendelea na ushahidi.
“SIFAHAMU MIPANGO YA CHADEMA KUHUSU VURUGU”
Katika dodoso jingine, Wakili Katuga alimuuliza Mnyika kuhusu madai ya kuwepo kwa mipango ya vurugu kabla na wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.
Mnyika alisema hafahamu mipango hiyo.
Alipoulizwa kuhusu madai kwamba baadhi ya wanachama waliwahi kuzungumza na waandishi wa habari na kueleza kuwa kulikuwa na mipango iliyopangwa na kuratibiwa na chama, Mnyika alisema hafahamu.
Pia alisema hafahamu madai ya kuwepo kwa mifumo maalumu ya mawasiliano ambayo ingetumika iwapo mitandao ya simu ingezimwa.
MNYIKA AULIZWA KUHUSU VURUGU ZA UCHAGUZI
Katuga alimuuliza Mnyika kama anafahamu kuwa vurugu za siku ya uchaguzi zilidaiwa kuwa zilipangwa na kuratibiwa.
Mnyika alisema alisikia kuhusu madai hayo.
Alipoulizwa kuhusu watu waliokamatwa kuhusiana na vurugu hizo, Mnyika alisema anafahamu kuwa baadhi yao walikamatwa na baadaye wakaachiwa.
Hata hivyo, alipohojiwa kuhusu madai kwamba watuhumiwa walifanya fujo kituoni kutokana na kauli za kiongozi wao, Tundu Lissu, Mnyika alisema hafahamu.
LISSU AOMBA MWENENDO WA KESI
Baada ya kesi kuahirishwa, Tundu Lissu aliomba apewe mwenendo wa kesi ili aweze kuusoma akiwa aliko.
Upande wa Serikali unatarajiwa kuendelea na dodoso kwa Mnyika kesho, huku kesi ikiendelea kufuatiliwa kwa karibu kutokana na ushahidi unaohusu kauli za viongozi wa CHADEMA, uchaguzi wa mwaka 2025 na madai yanayohusiana na vurugu.
Nzengeli: Na ni kweli mlitoa elimu pale pale kwenye ufunguzi
Mnyika: Ni kweli elimu ilianza kutoka kwenye ufunguzi
Nzengeli: Wewe ni mtaalamu wa sheria au hujui sheria?
Mnyika: Mimi sio mtaalamu wa sheria
Nzengeli: Nitakuwa sahihi nikisema huna utaalamu wowote wa kuchambua hati yoyote ya mshitaka
Mnyika: Ninaweza kuchambua uzoefu wa kutosha wa siasa
Nzengeli :Kama huna sema kama unao sema
Mnyika: Sina
Nzengeli : Kama mtu anauona uchaguzi ni wa haki na uhuru na unageuka kuwa sio wa haki kwa kuwa nyie chadema mmeamua
Mnyika: Akikubaliana na msimamo wetu
Nzengeli: Kama hajakubaliana
Mnyika; Hayo ni maoni yake
Nzengeli: Nimemaliza namualika Job Mrema amalizie waheshimiwa majaji Ahsante
Job : Waambie majaji hii kamusi hii inasemaje hapo juu kwenye kichwa cha habari
Mnyika: Kamusi kuu ya kiswahili Job Toleo la ngapi Mnyika toleo la tatu mwaka 2022
Job : Kwa mujibu wa lichosoma utafiti ulifanywa na nani kuandaa hiyo kamusi
Mnyika : Baraza la kiswahili la taifa
Job: Bakita ndio wamepewa mamlaka ya kufanya utafiti huo
Mnyika: Kwa Tanganyika
Job: Umeulizwa maswali mengi ukawa unasoma kwenye kamusi je ni hiyo uliyoishika hapo toleo la tatu
Mnyiaka: Ndio ndio hii
Job: Unakubaliana mimi kamusi hiyo ndio chombo rasmi cha kutoa tafsiri sahihi ya lugha ya kiswahili
Mnyika: Ni Rasmi ila sio nakala pekee
Job: Mimi sijakuuliza pekee
Mnyika :Hapana
Job: Ni sahihi umeiuizwa kuhusu michango ya tone tone ukasema mmekusanya milioni 302 pesa za Tanzania kuna michango mingine?
Mnyika sina takwimu kamili
Job: Ni kweli kwamba mshaanza kutumia michango ya tone tone na inetumika kiasi gani
Mnyika: Michango hiyo inatumika kwa lengo mahususi na ni michango ya baraza kuu la chama
Job: kama nimekusikia vizuri uliulizwa majukumu yako kama katibu mkuu wa chadema ulishindwa kuyataja ni kweli
Mnyika: hapana sio kweli
Job: Wewe kama mtendaji wa chama una majukumu gani
Mnyika: Msimaizi shughuli zote za kila siku za chama
Job: Kama ndio hivyo ndugu shahidi kama ndio ukweli ni sahihi kwamba umeulizwa maswali mengi ya kiutendaji na unasema hujui
Mnyika: Sio kweli mengi nimejibu ndio isipokuwa machache ambayo ninahitaji uelewa zaidi
Job: Unafikiri ni sahihi chadema kuwa na mtendaji mkuu asiyejua majukumu yake
Mnyika: Ninajua ninachofanya
Job: Nitakuwa sahihi nikesema ukatibu wako mkuu umekuwa wa kusaidiwa saidiwa na ni kama ahsante kwa mwenyekiti wa chadema
Mnyika : Sio sahihi
Job: Je ni sahihi katika utendaji wako umekuwa ukibebwa na mwenyekiti
Mnyika: Hapana
Job: Je ni sahahi hata kizimbani umeshindwa kujieleza mwenyekiti akaja kukunongoneza
Mnyika sio kweli
Job: Ndugu shahidi utakubaliana na mimi kwamba vyama vya siasa vilivyosajiliwa vinatakiwa kufuata sheria za nchi hii kanuni katiba za vyama husika
Mnyika: Ni sahihi Job sasa waambie waheshimiwa majaji nini maana ya fujo ni nini
Mnyika: Fujo ni Fujo
Job; Haya waambie waheshimiwa kwa mujibu wa kamusi uliyo nayo hapo
Mnyika: Bila kuwepo kwa utaratibu mzuri au mpango, hovyo hali ya ghasia na machafuko
