×

Global Yatoa Zawadi Kwa Wajasiriamali Arusha

  SHINDA NYUMBA (2)

Mratibu wa semina ya wajasiriamali na mwakilishi wa Global Publishers Kanda ya Arusha, Chocks Francisco Chokala (mwenye suti)  akiwa  na baadhi ya wajasiriamali huko Arusha katika Hoteli ya New Safari.

SHINDA NYUMBA (3)

…Akiendelea kusalimiana na wajasiriamali hao.

SHINDA NYUMBA (4)

Mwalimu wa wajasiriamali, James Mwagamba (kushoto) akiwa na Francisco Chokala.

SHINDA NYUMBA (1)

Wajasiriamali wakiwa katika picha ya pamoja baada ya semina hiyo.

KAMPUNI inayochapisha magazeti pendwa Tanzania, Global Publishers, Jumamosi ilimwaga zawadi mbalimbali kwa washiriki wa semina ya wajasiriamali iliyofanyika Jumamosi iliyopita katika hoteli ya New Safari jijiniArusha.   Mratibu wa Semina hiyo, Chocks Francisco Chokala, aliishukuru kampuni hiyo kwa kuijali jamii na kwa kuendesha bahati nasibu mbalimbali ikiwepo ambayo msomaji atajipatia nyumba kwa kujaza kuponi iliyo katika magazeti yote ya Global.  Shindano hilo la nyumba linamalizika mwisho wa mwezi huu, ambapo msomaji mmoja atabahatika na kupata sifa ya kuitwa “baba au mama mwenye nyumba”!

Leave a Comment