The House of Favourite Newspapers

Man U Walipa Kisasi kwa Man City, Waiondoa EFL

man-u MANCHESTER, ENGALD: Manchester United walifika hatua ya robo fainali katika Kombe la EFL baada ya kuwalaza mabingwa watetezi Manchester City kwenye debi iliyochezewa uwanja wa Old Trafford.

Juan Mata alifunga bao la pekee mechi hiyo baada ya kupata mpira kutoka kwa mshambuliaji Zlatan Ibrahimovic.

man-u1Paul Pogba alikuwa amegonga mlingoti kwa kombora kali awali na kusisimua mechi hiyo kipindi cha pili.

Kipindi cha kwanza kilikuwa kikavu bila upande wowote kupata kombora la kulenga goli.

Manchester United sasa watakutana na West Ham ambao waliwalaza Chelsea 2-1.

Ushindi huo wa United ulikuwa wao wa pili katika mechi tano, na wa nne kwa Jose Mourinho katika mechi 18 alizokutana na Pep Guardiola.

Comments are closed.