Alichosema Kocha Yanga Baada Ya Ushindi – Video
Kocha anayeshika nafasi ya Mkuu wa Yanga, Noel Mwandilabaada ya mechi dhidi ya Mtibwa Sugar amewapongeza wachezaji wake kwa kuibuka na ushindi.
Mabao ya Yanga yalifungwa na Heritier Makambo dakika ya 31 akiunganishwa kwa kichwa krosi ya Gadiel Michael, huku Kelvin Yondani akipigilia msumari wa mwisho dakika ya 40 kwa mkwaju wa penalti baada ya Mrisho Ngassa kuchezewa madhambi eneo la hatari na Issa Rashid ‘Baba Ubaya’.
Kipindi cha pili, timu zote zilikuwa zikishambuliana kwa kushtukiza ambapo dakika ya 72, Mtibwa walijipatia bao moja kupitia kwa Haruna Chanongo na mpaka mwamuzi kutoka Singida, Meshack Sud anapuliza filimbi ya mwisho, Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 2-1.
Comments are closed.