The House of Favourite Newspapers

Alichosema Kocha Yanga Baada Ya Ushindi – Video

Kocha anayeshika nafasi ya  Mkuu wa Yanga, Noel Mwandilabaada ya mechi dhidi ya Mtibwa Sugar amewapongeza wachezaji wake kwa kuibuka na ushindi.

 

Mabao ya Yanga yalifun­gwa na Heritier Makambo dakika ya 31 akiunganishwa kwa kichwa krosi ya Gadiel Michael, huku Kelvin Yon­dani akipigilia msumari wa mwisho dakika ya 40 kwa mkwaju wa penalti baada ya Mrisho Ngassa kuchezewa madhambi eneo la hatari na Issa Rashid ‘Baba Ubaya’.

 

Kipindi cha pili, timu zote zilikuwa zikisham­buliana kwa kush­tukiza ambapo dakika ya 72, Mtibwa walijipa­tia bao moja kupitia kwa Haruna Chanongo na mpaka mwa­muzi kutoka Singida, Meshack Sud ana­puliza filimbi ya mwisho, Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 2-1.

KOCHA MTIBWA Akataa Kuwapa Neno la Mwisho Mashabiki

Comments are closed.