The House of Favourite Newspapers

BILIONEA WA FACEBOOK APATA MTOTO WA PILI

0
Marc Zuckerberg na familia yake.

MKE wa Bilionea mwanzilishi na mmiliki wa mtandao maarufu duniani wa Facebook, Marc Zuckerberg ambaye ni daktari wa watoto nchini Marekani amejifungua mtoto wa kike juzi Jumatatu, Agosti 28, usiku.

Mtoto huyo ambaye ni wa pili kwa bilionea Zuckerberg na mkewe Priscilla Chan, amepewa jina la August.

Baada ya August kuzaliwa, Zuckerberg ameandika barua ya wazi kwa mtoto wao wa kwanza ambauye pia ni wa kike, Max aliyezaliwa mwaka 2015 akimuasa kucheza na mdogo wake.

 “Mimi na Priscilla tuna furaha sana kwa kumpata mtoto wetu August. Tumemuandikia barua  kuhusu ulimwengu tunaamini atakua na tunaamini hatakua haraka haraka” ameandika bilionea huyo katika ukurasa wake wa Facebook.

Makamba, Shaka, Shigongo, Sarungi, Marsha Kukutana Kwenye Meza ya Wazalendo


Leave A Reply