The House of Favourite Newspapers

IGP Sirro: Nitatoa Majibu Mauaji Kibiti Muda si Mrefu

1

 

Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro amesema muda si mrefu atatoa majibu ya suala la mauaji yanayotokea mkoani Pwani.

IGP Sirro amesema hayo leo (Julai 5) wakati wa makabidhiano ya magari manne ya polisi yaliyotolewa msaada na Kampuni ya Great Wall Motors and Haval.

 

“Si kawaida yangu kusemasema ila muda si mrefu nitatoa majibu ya mauaji ya Pwani. Sisi Watanzania hatujazoea mambo ya fujo fujo, wale waliotumwa kwa ubaya ubaya sisi tunawajibu vibaya vibaya,” amesema IGP Sirro.

Tangu Mei mwaka jana yalipoibuka mauaji ya kutumia risasi katika wilaya za Kibiti, Mkuranga na Rufiji mkoani Pwani, takriban watu 37 wameuawa wakiwamo askari polisi na viongozi wa Serikali za Mitaa.   

 

Kamishina wa Polisi Kitengo cha Fedha na Usafirishaji, Albert Nyamuhanga amesema magari hayo yenye thamani ya Sh120 milioni kila moja, yatasaidia kupambana na uhalifu nchini.

“Kupatikana kwa magari haya kumeokoa fedha nyingi katika bajeti ya Serikali, hivyo wadau hawa wameunga mkono juhudi za polisi kukabiliana na uhalifu,” amesema.

 

Mkurugenzi Mkuu wa Great Wall Motors and Haval, Jianguo Liu amesema magari hayo ni pongezi kwa kazi inayofanywa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na Jeshi la Polisi.

“Tunaunga mkono juhudi za polisi za kutunza amani na usalama wa raia,” amesema Liu.

 

1 Comment
  1. […] kupoteza muda? Watu watakusema? Au unaogopa kushindwa? Uhalisia ni kwamba, wakati mwingine huwa tunafikiria watu […]

Leave A Reply