The House of Favourite Newspapers

CARDI B AONGOZA KATIKA KUWANIA TUZO NYINGI BET 2019


MWANAMUZIKI, Cardi B ameongoza katika wasanii wanaowania tuzo nyingi za BET 2019 katika vipengele saba, Drake vipengele vitano, Beyonce, Travis Scott na J. Cole vipengele vinne, Bruno Mars, 21 Savage, Childish Gambino, H.E.R na Ella Mai vipengele vitatu.
Kwenye kipengele cha Best Male Hip-Hop Artist marehemu Nipsey Hussle anawania tuzo hiyo akiwa na wasanii J. Cole, Travis Scott, Meek Mill, 21 Savage na Drake.

Tuzo hizo za BET Awards 2019 zinatarajiwa kuanza kutolewa Jumapili Juni 23, katika ukumbi wa Microsoft Theater mjini Los Angeles.

Comments are closed.