The House of Favourite Newspapers

CHRIS BROWN ATHIBITISHA UJIO WA NGOMA YAKE NA DRAKE

MWANAMUZIKI wa marekani Chris Brown ametoa ahadi kwa mashabi wake ya kuwaletea nyimbo ya pamoja na rapa Drake, baada ya wawili hao kuonekana wakiwa na bifu kwa muda mrefu na kuripotiwa kuwa chanzo cha bifu kati yao ni mwanadada Rihanna.

Mei 5, mwaka huu kwenye birthday yake Chris Brown aliongelea kuhusu kolabo yake na Drake mashabiki wengi hawakuamini, kupitia ukurasa wake wa instagram alithibitisha hilo na kuandika maneno SUMMER TIME BOUT TO GET ALOT HOTTER! ( msimu huu wa majira ya joto joto litaongezeka zaidi). Chris Brown na Drake mpaka sasa hawajawai kuongelea tofauti zao.

Comments are closed.