The House of Favourite Newspapers

Ciara Yamkuta

HUENDA mwaka ukawa umeanza vibaya kwa staa wa muziki wa R&B, Ciara baada ya kufanya vibaya kwenye mauzo ya albamu yake kwa kuambulia kuuza kopi 100 tu hadi sasa.

 

Hivi karibuni, Ciara aliachia albamu yake ya saba, Beauty Marks lakini ndani ya wiki chache ilikuwa imeuza nakala 100 ambazo ni za chini kuliko hadhi yake na haijawahi kumtokea hali hiyo.

 

Licha ya kutoa nyimbo tano kutoka katika albamu hiyo ambazo ni Level Up, Freak Me, Dose, Greatest Love na Thinkin Bout You ambazo zimekimbiza kinoma lakini albamu hiyo imeshindwa kuuza wala kuingia hata kwenye chati mojawapo kubwa duniani.

 

Hili ni pigo kwa Ciara ambaye tangu aanze muziki hajawahi kukutana na hali kama hiyo.

 

Alipoanza rasmi muziki mwaka 2004 aliachia albamu yake ya kwanza iitwayo Goodies ambapo kwa wiki ya kwanza tu alivunja rekodi ya kuuza nakala zaidi ya 124,000.

Comments are closed.