Dkt. Mwigulu Awasili Zanzibar Kwa Uzinduzi wa Miradi ya Maendeleo

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba, amewasili Zanzibar leo, Januari 4, 2026, kwa ziara ya kikazi.
Katika ziara hiyo, Dkt. Mwigulu atashiriki kwenye uzinduzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo, ikiwa ni sehemu ya shamrashamra zinazoelekea kilele cha maadhimisho ya miaka 62 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Miradi hiyo inalenga kuimarisha huduma za kijamii na kuchochea maendeleo kwa wananchi.


