The House of Favourite Newspapers

Familia Yakomalia Ndoa ya Jokate na Kiba

1
Alikiba.

 

DAR ES SALAAM: Familia ya nyota wa Muz­iki wa Kizazi Kipya, Ali Kiba, imesema inahitaji ndoa kati ya kijana wao na mrembo namba mbili wa mwa­ka 2006, Jokate Mwegelo ifanywe mara moja, Risasi Mchanganyiko limeambiwa.

 

Katika mahojiano maalum na mama mzazi na dada yake kwa nyakati tofauti jijini Dar, wanafamil­ia hao walisema hivi sasa ni wakati muafaka kwa Ali Kiba kupata jiko kwani umri umefika na hakuna ali­chobakisha katika maisha yake ya ujana.

 

“Mimi kama mzazi, ninaona muda wa Ali kuoa sasa umefika maana kama ni maisha ya ujana amesha­fanya kila kitu, ana watoto wanne na kila mmoja na mama yake, ni vi­zuri sasa akachukua mke ili aweze kuwalea hawa watoto wake,” al­isema mama huyo alipozungumza na Risasi Mchanganyiko nyumbani kwake hivi karibuni.

Jokate.

 

“Mimi kama mzazi huu ndiyo msimamo wangu, ninamtaka ata­fakari na kuchukua uamuzi mara moja, maana ingawa siyo vizuri kwa mzazi kumpangia mtoto wake cha kufanya, lakini inapofikia suala la kuoa ni muhimu ukasimama na ku­toa msimamo, wakati wa kuoa ume­fika,” alisema mama huyo.

 

Alipoulizwa juu ya mwanamke gani anadhani ndiye anafaa kuwa mkwewe, alisema hawezi kulijibu swali hilo, kwa kuwa uamuzi hasa wa nani anafaa upo mikononi mwa msanii huyo, ingawa angefurahi kama angetokana miongoni mwa wasichana ambao wamekuwa wak­ihusishwa naye.

 

“Mimi muda mwingi niko nyum­bani, labda ndugu zake wanaweza kujua msichana anayefaa kwa sababu wanakuwa wote muda mwingi, mimi kitu cha msingi ninachotaka ni yeye sasa aoe,” al­isema mama huyo aliyekiri kuwa licha ya mwanaye kusemwa kuwa na watoto wanne, yeye amewahi kumuona mmoja tu.

Jokate na Alikiba.

 

Wakati mama yake mzazi akitoa kauli hiyo, dada wa mwimbaji huyo wa kibao cha Aje, Zabibu alisema msichana pekee ambaye familia ingependa kumuona akiolewa na kaka yake ni Jokate Mwegelo, na kumuombea wakati wowote awe wifi yake.

 

Zabibu, ambaye amekuwa ni mtu wa karibu wa Jokate kwa kipindi kirefu, alisema mrembo huyo ambaye pia ni msanii na mjasiriamali, ni msichana mwenye upendo na angefurahi sana kama ingetokea kuolewa na kaka yake mara moja.

“Mimi namchukulia Jokate kivingine kabisa, ni msichana mwenye busara zake na amekuwa kama mshauri wangu wa karibu mno, ningetamani angekuwa mke halali wa kaka yangu kwa sababu ana vigezo vyote vya kuwa hivyo,” alisema Zabibu.

 

“Kwa kuwa kaka yangu bado hajaoa, ninaomba kila kukicha na­fasi hiyo ichukuliwe na Jokate kwa sababu ni mwanamke anayestahi­li kuipata nafasi hiyo ya kuwa wifi yangu,” alisema Zabibu ambaye pia ni rafiki wa mastaa wengi.

 

Risasi Mchanganyiko lilijaribu kumtafuta kaka mtu, Ali Kiba ili kuzungumzia maoni hayo ya watu wa familia yake, lakini hakupatika­na kupitia simu yake ya mkononi na hata Jokate alipotumiwa ujumbe mfupi wa maneno kupitia Mtandao wa WhatsApp, hakujibu ingawa swali hilo lilionekana ku­somwa.

 

IMELDA MTEMA | RISASI MCHANGANYIKO

1 Comment
  1. […] kurejea nchini ili niwe karibu na familia yangu, pia namshukuru sana mke wangu kwa kuitambulisha ngoma yangu kwa Watanzania, na kuniwakilisha […]

Leave A Reply