
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga anawatangazia Watanzania wenye sifa kuomba ajira za nafasi nne (04) baada ya kupokea kibali kutoka Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora. Bonyeza hapa >>NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA IGUNGA 
1.0 MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II
Idadi ya Nafasi: 04
1.1 MAJUKUMU NA KAZI
Mwajiriwa atakuwa na jukumu la:
-
Kuchapa barua, taarifa na nyaraka za kawaida na za siri.
-
Kupokea wageni, kuwasaidia na kuwaelekeza sehemu husika.
-
Kutunza kumbukumbu za matukio, miadi, wageni, vikao, safari na ratiba za kazi za Mkuu wake.
-
Kutafuta majalada na nyaraka zinazohitajika katika utekelezaji wa majukumu.
-
Kupokea na kusambaza majalada kwa Maafisa wa Idara/Vitengo husika.
-
Kukusanya, kutunza na kurekebisha majalada na nyaraka.
-
Kuandaa dondoo na maandalizi ya vikao mbalimbali.
-
Kuandaa orodha ya mahitaji ya vifaa vya ofisi.
-
Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na msimamizi wake.
1.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Mwombaji anapaswa kuwa:
-
Mhitimu wa Kidato cha Nne (Form IV) au Kidato cha Sita (Form VI).
-
Mwenye Stashahada (Diploma) ya Uhazili au Cheti cha NTA Level 6 ya Uhazili kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali.
-
Amefaulu Hatimkato ya Kiswahili na Kiingereza kwa kasi ya maneno 100 kwa dakika moja.
-
Mwenye ujuzi wa matumizi ya programu za kompyuta za ofisi kama: Word, Excel, PowerPoint, Internet, E-mail na Publisher.
1.3 NGAZI YA MSHAHARA
-
TGS C
2.0 MASHARTI YA JUMLA
-
Mwombaji awe Raia wa Tanzania mwenye umri wa miaka 18–45.
-
Waombaji wenye ulemavu wanahamasishwa kuomba na wanapaswa kubainisha aina ya ulemavu kwenye mfumo wa ajira.
-
Waombaji waambatanishe CV yenye anuani, namba za simu, barua pepe na majina ya waamuzi (referees) watatu.
-
Provisional results, testimonials au statement of results HAVITAKUBALIWA.
-
Cheti cha kuzaliwa kiwe kimehakikiwa na Mwanasheria/Wakili.
-
Waombaji waliowahi kuachishwa Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kwa kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.
-
Waombaji walioko kwenye Utumishi wa Umma wazingatie taratibu husika za uwasilishaji wa maombi.
-
Vyeti vyote vya elimu na taaluma viwe vimehakikiwa na Mwanasheria/Wakili.
-
Waombaji waliosoma nje ya nchi wahakikishe vyeti vimethibitishwa na NECTA, NECTVET au TCU.
-
Kughushi taarifa au sifa kutachukuliwa hatua za kisheria.
-
Barua ya maombi iandikwe kwa Kiswahili au Kiingereza.
3.0 JINSI YA KUOMBA
-
Maombi yote yawasilishwe kwa njia ya kielektroniki kupitia:
👉 https://portal.ajira.go.tz -
Barua ya maombi ielekezwe kwa:
Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
S.L.P. 19
IGUNGA
📅 Mwisho wa kupokea maombi: 01 Januari, 2026
Imetolewa na:
MKURUGENZI MTENDAJI (W)
HALMASHAURI YA WILAYA YA IGUNGA

