Hatimaye Vee Money, Jux Uso kwa Uso Jukwaa la Fiesta Arusha (Video)
WASANII wa Bongo Fleva ambao pia wamekuwa wapenzi kwenye mahusiano yao kwa miaka kadhaa huku wakidai kuachana hivi karibuni, Juma Jux na Vanesa Mdee ‘Vee-Money’ juzi Jumamosi walikutana pamoja kwenye Jukwaa la Shoo ya Fiesta iliyofanyika mkoani Arusha.
Baada ya kushuka jukwaani, Jux na Vee Money kila mmoja alikuwa alikuwa na haya ya kusema.