The House of Favourite Newspapers

Huyu Ndo Aliyemtabiria Mama Samia Urais Miaka 15 Iliyopita

0

 

ALIYEKUWA Mtabiri maarufu Afrika Mashariki, Shehe Yahya Hussein aliitisha mkutano wa wahariri na waandishi wa habari mwaka 2006 na kuzungumzia utawala wa Rais Jakaya Kikwete ukiwa na umri wa mwaka mmoja tu.

 

Baada ya kuzungumza hayo nilipata nafasi ya kumuuliza. Je Tanzania baada ya Kikwete inaweza kupata rais mwanamke?

 

Shehe Yahya alinijibu:

“Baada ya vipindi viwili vya Rais Kikwete atakuja rais ambaye ni mweusi mchapa kazi lakini mchekeshaji sana, hata hivyo atatawaka kwa kipindi kifupi tu hapo ndipo Tanzania itapata rais mwanamke.”

 

Wahariri na waandishi waliguna kuonesha kutokubaliana naye wakiwemo wahariri wakongwe Hemedi Kimwaga, Yasini Sadiki, Magnus Mahenge na wengine ambao siwezi kuwakumbuka.

 

Shehe Yahya baada ya kuona tunambishia alichukua ubao kama ule wa darasani na mkononi alishika kutabu kilichoandikwa Astrology: Monthly numerology, akaanza kufanya hesabu kwa fomula anazojua yeye na akatuambia kwamba kwa Jakaya inaonesha atamaliza muda wake wa miaka kumi na lakini ajaye ataongoza kwa kipindi kifupi.

 

Tulimuuliza ataongoza kwa muda mfupi kwa sababu gani, alisema hayo mengine yeye hawezi kujua lakini akasisitiza kwamba hivyo ndivyo itakavyokuwa. Tulitawanyika pale kila mmoja akiwa anaona kama amepigwa ‘changa la macho’.

 

 

Lakini sasa nimeng’amua kwamba kumbe alikuwa akimtabiria mama Samia bila yeye mama kujua tulichokuwa tunafanya.

 

HAKIKA SHEHE YAHYA ALIKUWA MNAJIMU WA KWELI.

Kumbuka haya yanatokea baada ya miaka 15 ya utabiri wake na mtabiri akiwa katangulia mbele za haki. Sheh Yahya alifariki mwaka 2011. Mungu ampe raha ya milele na amnusuru na adhabu ya kaburini.

 

ANAANDIKA MHARIRI WA GAZETI LA UWAZI, ELVAN STAMBULI

 

🔴#LIVE: KUAGWA Kwa MAGUFULI, RAIS SAMIA SULUHU AONGOZA MAELFU KUTOA HESHIMA ZA MWISHO..

Leave A Reply