Kutoka katika Shule ya Msingi, Lucky Vincent, Karatu.
Ni siku moja tangu watoto watatu, Wilson, Sadia pamoja na Doreen wawasili nchini. Watoto hao walinusurika katika ajali ya gari miezi mitatu iliyopita walipokuwa wakienda Karatu katika ziara ya masomo. leo wanakaribishwa rasmi shuleni kwao.
Pia, mnara maalumu wa kumbukumbu ya watoto 32, walimu wawili, na dereva mmoja walioaga dunia kwenye ajali hiyo, umezinduliwa rasmi ikiwa ni ishara ya kuwaenzi na kuwakumbuka daima.
Wakati wa uzinduzi wa mnara, wazazi, walimu na wanafunzi wa shule hiyo pamoja na walionusurika, wameshindwa kujizuia na kujikuta wakiangua vilio walipokuwa wakiweka mashada ya maua kwenye mnara.
Mwandishi: Edwin Lindege | GPL