RAIS Dkt. John Pombe Magufuli ‘JPM’ amesema yeye kama kiongozi mkuu wa nchi haogopi vitisho vya kufungwa ama kushtakiwa vinavyotajwa na baadhi ya wanasiasa baada ya kuwashughulikia wawekezaji wanaokiuka mikataba na kuhujumu uchumi wa nchi na badala yake ataendelea kuwatetea Watanzania wanyonge ili wapate haki yao.
JPM ameyasema hayo leo wakati akiwahutubia wananchi wa Kigoma katika Uwanja wa Lake Tanganyika mjini humo.
“Hii nchi imejaa mafisadi, wamo wa CCM, Chadema, CUF, ACT, wazungu na wengine hawana chama.
“Siogopi kufungwa, kama mliniteua niwatetee, nitawatetea kwa nguvu zangu zote juu ya majizi, tumeibiwa vya kutosha, madini yetu yanachimbwa yanapelekwa nje na hatupati kitu.
“Wengine wamelipwa pesa ili kupinga tusichukue hatua dhidi ya majizi, nawaambia mimi kama rais nimejitoa kufa na kupona mpaka nihakikishe mali za Watanzania wanyonge haziibiwi na haki yao wanaipata.
“Watambue kwamba sitafungwa badala yao majizi ndiyo yatafungwa. Ilikuwa lazima tubadilishe sheria zetu hatuwezi kuendelea kuibiwa rasilimali zetu,” alisema Rais Magufuli.
Yaliyojiri kwenye mkutano huo.
#JPMKigoma: Mhe Rais @MagufuliJP licha ya kwamba upinzani tunatoka vyama tofauti lakini maendeleo hayana vyama, tunakuunga mkono-@zittokabwe pic.twitter.com/iSae4TAFCj
— Global Publishers (@GlobalHabari) July 22, 2017
#JPMKigoma: Tangu awamu ya 5 iingie madarakani, meli ya MV Liemba imekuwa ikifanya kazi na kuingiza faida kubwa tofauti na zamani- @MbarawaM pic.twitter.com/PZ5RFKRR2O
— Global Publishers (@GlobalHabari) July 22, 2017
#JPMKIgoma: Julai 31, 2017 ukarabati wa shule kongwe ya Sekondari Kigoma utaanza kufanyika na wakala wa ujenzi Tanzania. –@JoyceNdalichako pic.twitter.com/MSusJpWhpU
— Global Publishers (@GlobalHabari) July 22, 2017
#JPMKigoma: Haiwezekani miaka zaidi ya 50, mkoa wa Kigoma barabara za lami bado ni tatizo. Nimemuelekeza kuanzia mwezi ujao atangaze zabuni.
— Global Publishers (@GlobalHabari) July 22, 2017
#JPMKigoma: Hii nchi imejaa mafisadi, wamo wa CCM, Chadema, CUF, ACT, wazungu na wengine hawana chama. –@MagufuliJP https://t.co/qiUMMfhhFy pic.twitter.com/9g486wxI6M
— Global Publishers (@GlobalHabari) July 22, 2017
#JPMKigoma: Ninataka kutengeneza watumishi waaminifu na waadilifu. Tuhakikishe tunawasaidia Watanzania maskini. @MagufuliJP
— Global Publishers (@GlobalHabari) July 22, 2017
#JPMKigoma: Wengine walisema ndege tulizonunua zinakimbia polepole kama bajaji, niliwaambia wapande za jeshi zenye spidi kubwa. @MagufuliJP. pic.twitter.com/zEn5iTvP6G
— Global Publishers (@GlobalHabari) July 22, 2017
#JPMKigoma: Nilwateua Prof. Mkumbo na Anna Mghwira kwa sababu ni wachapa kazi na maendeleo hayana chama. @MagufuliJP
— Global Publishers (@GlobalHabari) July 22, 2017
#JPMKigoma: Siogopi kufungwa, kama mliniteua niwatetee nitawatetea juu ya majizi. Tumeibiwa sana, madini yetu yanachimbwa yanapelekwa nje.
— Global Publishers (@GlobalHabari) July 22, 2017
#JPMKigoma: Kila jambo lina mwisho wake, tumewapokea sana wakimbizi tangu 1994, ifike wakati Warundi warudi Burundi sasa. @MagufuliJP
— Global Publishers (@GlobalHabari) July 22, 2017
#JPMKigoma: Kuhusu wananchi walionyanyua mabango yenye ujumbe, Rais @MagufuliJP amesema atamtuma waziri Lukuvi ili kutatua migogoro ya ardhi
— Global Publishers (@GlobalHabari) July 22, 2017
Rais @MagufuliJP amewaagiza RC Kigoma na DC wapange kutatua matatizo ya wananchi wao yatakayowashinda wampelekee awapangie mawaziri husika
— Global Publishers (@GlobalHabari) July 22, 2017
[…] ya ‘Magufuli Baki’ iliyoanzishwa karibuni na mwanaharakati ambaye pia aliwahi kuwa mgombea ubunge wa Jimbo la […]