The House of Favourite Newspapers

Man City Yampiga Pini Aguero

Sergio Aguero

STRAIKA wa Manchester City anayeo-ngoza kwa kufunga mabao mengi zaidi klab-uni hapo, Sergio Aguero amejihukumu baada ya kukubali kusaini mkataba mpya wa kuendelea kuichezea timu hiyo hadi mwaka 2021.

 

Aguero anashika rekodi ya kuwa mfungaji bora wa muda wote ambayo awali ilidumu kwa miaka 78 baada ya kuwekwa na Eric Brook, amesaini mkataba ambao utamwezesha kulipwa pauni 220,000 kwa wiki.

 

Staa huyo wa zamani wa Atletico Madrid alizungumza baada ya kusaini mkataba huo kwa kusema: “Wazo langu lilikuwa ni kudumu hapa kwa miaka 10, nimekuwepo hapa kwa miaka saba hivyo nimepata nafasi ya kutimiza kile nilichokuwa nikikiwaza cha kudumu kwa miaka 10.

 

“Nina furaha kubwa kwa kuwa wananihudumia vizuri tangu siku ya kwanza, nina furaha na kila kitu cha klabuni hapa, wachezaji wenzangu, makocha na viongozi.”

 

Aguero, alijiunga na Man City akitokea Atletico Madrid mwaka 2011, lakini chini ya utawala wa Kocha Pep Guardiola alilazimika kusubiri muda kuzoea aina ya ufundishaji wake.

Comments are closed.