The House of Favourite Newspapers

MANCHESTER CITY WABABE EPL, WABEBA KOMBE, WAIKALISHA LIVERPOOL

USHINDI wa mabao 4-1 dhidi ya Brighton leo uwanja wa Amex umetosha kuwarejeshea ubingwa wao msimu huu baada ya kufikisha jumla ya pointi 95.
Mabao ya Manchester City yalipachikwa kimiani na Sergio Aguero dk ya 28, akisawazisha bao lililofungwa na Glenny Murray dk ya 27, liliamsha mvua ya mabao ambayo yalifungwa na Laporte 38, Maherz 63 na Gundogan 72.
Licha ya Liverpool kushinda leo mabao 2-0 mbele ya Wolves mchezo uliochezwa uwanja wa Anfield hayajawasiaidia kwani wanamaliza wakiwa nafasi ya pili na pointi zao 94.
Mabao ya Liverpool yalipachikwa na mshambuliaji Sadio Mane mbaye naye anafikisha mabao 22 kwa watupiaji sawa na Sadio Mane, Pierre Aubameyang wa Arsenal.

Comments are closed.