Mke wa Wayne Rooney Atarajia Mtoto wa Nne
Mke wa aliyekuwa mshambuliaji wa Manchester United, Wayne Rooney, Coleen hivi karibuni kupitia ukurasa wake wa Twitter wenye wafuasi milioni 1.25 amesema : “Nina furaha sana!!! ….. Sijawahi kukanusha habari hizi, lakini nilikuwa ninazilinda vyema!! Nimepimwa na kuchunguzwa na kila kitu kiko sawa…Mtoto nambari 4 yupo njiani.”
Wayne, ambaye aliyehamia klabu ya Everton msimu huu, alisambaza ujumbe huo.
Coleen na Wayne walifunga ndoa mwaka 2008 kwa sasa wana watoto watatu wa kiume – Kai, wa miaka minane, Klay, wa miaka minne, na Kit, aliyezaliwa Januari 2016.
Katika mahojiano na jarida la New, alisema: “Nafikiria kumpata msichana. Nina familia kubwa, kwa hivyo ningetaka wasichana sawa na ninavyowataka wavulana.”