The House of Favourite Newspapers

Msako Mkali Kumtafuta Mwizi wa Chatu wa Kifalme

0

JESHI la Polisi nchini Uingereza limesema linaendesha msako mkali kumtafuta mwizi wa chatu wa kifalme ambao walichukuliwa kutoka katika eneo la Hillmorton eneo la Rugby, Jumamosi asubuhi.

 

Mwizi huyo anaaminika kuwapakia viumbe hao na kutoroka nao baada ya kuingia kwenye nyumba hiyo iliyoko Horne Close, kabla ya kupitia kwenye makaburi yaliyo karibu na eneo hilo.

 

Pamoja na nyoka, funguo na pesa pia viliibiwa, Polisi wa Warwickshire walisema. Wachunguzi walisema chatu hao wana alama za kibinafsi ambazo zinapaswa kuwafanya kutambulika kwa urahisi iwapo watatokea.

 

Polisi wanaamini kuwa mhalifu huyo aliwachukua viumbe hao kupitia makaburi ya Watts Lane kisha kukimbia eneo hilo na kutoa wito kwa yeyote aliyeona jambo lolote la kutia shaka katika eneo hilo kujitokeza.

Leave A Reply