Msanii Mpya wa Harmonize Aachia Dude la Kwanza – Video
MSANII mpya aliyetambulishwa na Mkurugenzi wa Lebo ya Konde Gang, Harmonize anayejulikana kwa jina la Ibrah, tayari ameachia wimbo wake wa kwanza akiwa chini ya lebo hiyo.
Wimbo huo ambao umepewa jina la ‘Nimekubali’ umefanywa na producer Kapipo, Ibrah alitambulishwa na Harmonize juzi Jumamosi, Aprili 11, 2020, ikiwa ni siku mbili kabla ya kuachia wimbo huu mpya.