Mtanzania Aliyetoroka Oman Afichua Mazito ‘Nilikuwa Napewa Sambusa, Mshahara Hakuna’” – Video

Mwanadada Farida Hamadi ni miongoni mwa wanawake waliokuwa wanaishi nchini Oman 🇴🇲, ambako walikwenda kufanya kazi za ndani lakini baadaye wakajikuta wakikwama katika mazingira magumu ya maisha.
Farida ni mmoja kati ya wanawake zaidi ya 16 waliokuwa wakiomba msaada ili kurejea nchini baada ya kukumbana na changamoto mbalimbali wakiwa ugenini.
Kupitia kipindi cha Mapito kinachorushwa na Global TV, Farida amefunguka na kueleza kwa kina maisha magumu aliyokuwa akipitia alipokuwa akifanya kazi nchini Oman.
Ameeleza kuwa hadi sasa, wanawake 9 tayari wamesharejea nchini, huku wengine wakiendelea kusubiri msaada.
Mwanadada huyo ameeleza zaidi kuwa Bosi wake alikuwa anampa sambusa moja lakini mshahara alikuwa anamnyima.
Ushuhuda wake umeibua hisia na kutoa funzo kwa jamii kuhusu changamoto za ajira za ndani nje ya nchi, hasa kwa wanawake.
Host @zali_mapito
Cameraman @zachariajuma0701

