Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe, leo Julai 10 amesitisha uteuzi wa mwenyekiti pamoja na wajumbe wote wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT) kuanzia leo kwa mamlaka aliyopewa na sheria ya BMT Na.12 ya 1967.
Mwakyembe ameeleza kuwa sababu ya kusitisha uteuzi huo inatokana na agizo alilopewa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliyemwagiza afanyie kazi mapitio na kulitathmini upya baraza hilo ili kujiridhisha na usimamizi wake kuhusu michezo.
Kutokana na kujiridhisha kwake kwamba usimamizi wa BMT si imara, amelivunja na ataliunda upya. Kwa sasa sekretarieti ya baraza hilo itaendelea kufanya kazi katika kipindi hiki ikishirikiana na wizara.
PICHA NA DENIS MTIMA | GLOBAL PUBLISHERS
Waziri wa Habari, Dkt Mwakyembe amesitisha uteuzi wa Mwenyekiti na wajumbe wote wa BMT kwa mamlaka aliyopewa na sheria ya BMT Na.12 ya 1967 pic.twitter.com/RkKiujRxRH
— Global Publishers (@GlobalHabari) July 10, 2017