The House of Favourite Newspapers

Nguruwe Abakwa Akisubiri Kuchinjwa

0

MKAZI wa Kijiji cha Mavanga kilichopo katika kata ya Mavanga wilayani Ludewa mkoani Njombe ambaye jina lake halijafahamika anashikiliwa na Jeshi la Polisi katika Kituo cha Mgalala kwa tuhuma ya kumbaka mnyama aina ya Nguruwe ambaye anamilikiwa na Afro Nyigu (31).

 

Afisa Mtendaji wa Kijiji hicho Ramadhani Kihanga amesema kuwa tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia Novemba 14, 2021 ambapo mtuhumiwa huyo alifika katika machinjio ya wanyama hao huku akiwa amelewa na kukuta nguruwe akiwa amefungwa kamba kwa maandalizi ya kuchinjwa ndipo kijana huyo alimvamia na kufanya nae mapenzi.

 

Amesema wakati akiendelea na tendo hilo mlinzi wa machinjio hiyo alikuwa ametoka kidogo na aliporejea alimkuta kijana huyo akiendelea kufanya kitendo hicho ambapo alimkamata na kumpigia simu balozi na mtendaji wa kijiji ambao walifika katika eneo hilo la tukio.

 

Amesema kuwa walipomuhoji kijana huyo sababu za kufanya kitendo hicho alidai ni maamuzi yake binafsi hivyo hapaswi kuulizwa ambapo viongozi hao wakamchukua na kumkabidhi mikononi mwa polisi.

 

“Kitendo alichokifanya huyu kijana mwenzetu ni cha kusikitisha sana! Tunaomba sheria ichukue mkondo wake ili iwe fundisho kwa wengine maana kama ameweza kufanya hivi kwa mnyama anaweza kufanya uharibifu hata kwa binadamu,” amesema Kihanga.

 

Akizungumza Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Njombe Hamiss Issa na mtandao huu amesema ni kweli tukio hilo lipo na kwa sasa Jeshi la Polisi linafanya uchunguzi wa tukio hilo na mtuhumiwa amehifadhiwa katika kituo cha Polisi Mgalala.

Leave A Reply