The House of Favourite Newspapers

PAM D AGEUKIA SINGELI

MSANII wa Bongo Fleva, Pamela Daffa ‘Pam D’ ameamua kugeukia muziki wa singeli na kuahidi kuliteka soko hilo, kwa kuwa anaamini muziki huo bado haujapata mwanamke anayeumudu.

 

Akipiga stori na Risasi Vibes, Pam D alisema yupo kwenye maandalizi ya mwisho ya kuachia wimbo wake wa singeli ambao amemshirikisha Msaga Sumu hivyo amejipanga vilivyo kuleta mapinduzi ya hali ya juu kwenye muziki huo.

 

“Nimeamua kuimba Singeli kutokana na ushawishi mkubwa nilioupata kwa Msaga Sumu maana ni mtu wangu wa karibu ambaye tunashauriana mengi, si kwamba nitaacha Bongo Fleva ila tu nataka kuwaonyesha mashabiki wangu kwamba muziki wa aina yoyote naweza kufanya na nikatusua,” alisema.

 Mayasa Mariwata

Comments are closed.