The House of Favourite Newspapers

Polisi Wamsaka Mke wa Mugabe

Polisi nchini Afrika Kusini imetoa amri ya kukamatwa kwa Grace Mugabe, mke wa aliyekuwa rais wa Zimbabwe Robert Mugabe ambaye anatuhumiwa kumshambulia na kumjeruhi mwanamitindo wa Afrika Kusini, Gabriella Engels, mwaka 2017.

 

Mwanasheria anayefanya kazi na shirika la kutetea haki za binadamu la AfriForum la huko Afrika Kusini, Garrie Nel amesema amethibitishiwa na Polisi kuhusu kutolewa kwa amri hiyo, na kuongeza kuwa ikiwa Bi. Mugabe atakanyaga kwenye ardhi ya Afrika Kusini atakamatwa.

Mwanasheria huyo vile vile ametaka mchakato wa kumtia mbaroni Grace Mugabe na kumsafirisha hadi Afrika Kusini uanze sasa.

 

Grace Mugabe anatuhumiwa kumpiga na kumjeruhi mwanamitindo Gabriella Engels kwenye hotel moja mjini Johannesburg Agosti mwaka 2017, lakini hakushtakiwa kwa sababu alikuwa na kinga ya kidiplomasia.

MAHAKAMAA YA WANANCHI kufungiwa kwa Diamond na Rayvanny

Comments are closed.