The House of Favourite Newspapers

PUNGUZA MAJI UGALI UIVE

NASHUKURU kwa wote mlionipongeza kwa kupata mafunzo ambayo hawakuyapata hapo awali, siyo wote wamepitia mafunzo ya utaratibu wa maisha wa jando au unyago.  Kutokana na kupokea maombi ya kina baba nao kuomba niwakumbuke katika ufalme wa mahusiano nami sina hiyana kwa vile wao ndiyo wapiga gitaa wetu sisi wachezaji tu. Hili lilikuwa swali ambalo naamini limekuwa sugu katika nyumba zetu kila kukicha kwa kina baba kupungua uwezo wa kufunga magoli ya mapema na akiishalipata huvua jezi na kujilaza nje ya uwanja.

Hii imekuwa ikiwaumiza sana kina mama sawa na kipa aliyefanya mazoezi ya kuzuia mashuti makali lakini baada ya mpira kuanza mshambuliaji akupigie shuti kama mate ya mlevi, inaudhi kwa kweli, shuuutuuuu! Kibaya zaidi anatoka nje ya uwanja na kukuacha ukiteseka na kukimbilia kujikanda na maji ya moto kila siku mwisho kutaota sugu na kuua virutubisho na kuondoa ladha.

Japo si mtaalamu sana wa mambo hayo lakini kuna kitu nilikutana nacho ambacho kilinipa somo na kuona kuna umuhimu wa kuwaeleza akina baba wengine nao wajaribu kutumia njia hii. Wapo niliowaelekeza na kukubaliana na nilichowafundisha, mmh naona mimacho imekutoka na kusubiri ujue ni mbinu gani za kukufanya angalau ulie machozi mawili na kumfurahisha mpenzio.

Shoga yangu alishawahi kunisimulia alivyokutana na mwanaume mmoja ambaye anasema ukimuangalia utajua hana kasoro yoyote basi kama kawaida akaingia kwenye shamba lake la minazi. Mwanamke akaanza kuukwea huku akitatalika kama bisi jikoni, kijana wa watu alijaliwa sura, nguvu na uwezo wa kuuyumbisha mnazi wake kimadaha na kumfanya ahisi raha ya ajabu.

Lakini kabla hajafikia madafu ili anywe maji yake, alilitoa dafu lake na kuyamwaga maji yake pembeni ambayo naye alikuwa na kiu nayo pia ndiyo yaliyomfanya aupande mnazi wake kwa kasi. Baada ya muda alimpandisha tena, kwa vile mzuka ulikuwa haujamshuka moto ulianzia uliposimamia, basi mwenzangu alijikuta akifika mwisho wa mnazi. Unajua alitumia njia gani kupata mbili za mkwezi?

Jamaa yule alimueleza kuwa kutokana na ugumu wa shughuli zake zimemfanya apungue uwezo wa kuangusha madafu mengi, kama dafu la kwanza angelipasulia ndani asingeweza kumfurahisha kwa vile mnazi usingeweza kusimama tena. Alisema maji mengi hayapiki ugali, ukipunguza maji lazima ugali utaiva lakini ukipika hivyohivyo lazima ukoroge uji. Kwa leo naomba niishie hapa, ni mimi Anti Naa Shangingi Mstaafu!

Comments are closed.