The House of Favourite Newspapers

Simba Wajiangalie Kwenye Kioo Kabla Hawajavurugana

SIMBA imesajili kikosi cha bei ghali, Simba ina kocha mkali kutoka Ubelg­iji, Simba ina mastaa wengi, Simba ni kama timu ya taifa, Simba kuna neema kutoka­na na uwepo wa Mo Dewji, Simba ndiyo mabingwa wa­tetezi, Simba wana Ofisa Habari anayejua kuongea…

 

Kuna sifa nyingi am­bazo unaweza kuzitoa kwa Simba hii ya sasa na kweli kwa kiasi fulani wanas­tahili kwa lengo ya soka letu la Tanzania na Af­rika Mashariki kwa jumla.

 

Ushiriki wao uwanjani katika michuano ya ki­mataifa haukuwa mzuri sana lakini hata walivyo­tolewa siyo kwa aibu au kama timu ambayo haikuwa na maandalizi bali ni matokeo ya kuzidiwa ki­dogo na wapinzani wao.

 

Ni kweli kama klabu im­ekuwa na neema nzuri kuliko ilivyokuwa kwa ma­jirani zao ambao ni wap­inzani wao wa jadi, Yanga. Hilo lipo wazi na halina ubishi lakini naitazama hali hii ambayo naweza kusema ni kama ‘ufalme’ wa Simba katika jicho la tatu na kuona kama ku­kokosekana umakini kuna tatizo kubwa linaweza kutokea hapo mbeleleni.

 

Pale juu katika aya ya kwanza niliweka nukta tatu nikimaanisha kuna sifa nyingi ambazo zi­naendelea wanastahili ku­pewa, lakini tayari kuna uchaguzi unakuja, upande wa pili ushindani huwa uwanjani nao umeanza kuonekana kuwa mkali.

Simba walipata suluhu dhidi ya Ndanda FC ya Mtwara, ni matokeo am­bayo hayakutegemewa na Wanasimba wengi hasa ikizingatiwa kuwa kikosi chao kiliingia kikiwa ka­mili, hakukuwa na kisin­gizio chochote, upande mwingine kocha wao msaidizi, Masoud Djuma ambaye imekuwa ikise­ma yupo kwenye ‘kaa la moto’ la kutimuliwa, naye alibaki Dar wakati mch­ezo ukichezwa Mtwara.

 

Baad aya matokeo hayo kumekuwa na lawama kadhaa kuhusu ubora wa kocha, japo ni mapema sana hilo kutokea lakini hiyo ndiyo kawaida ya mashabiki wa soka po­pote duniani hasa Tan­zania, huwa ni lazima watafute ‘wakufa’ naye.

Safari hii Simba wapo Mwanza, Djuma kabaki tena Dar, wao wanasema ni sehemu ya mipango yao, lakini hii inatokea Tanzania pekee, kocha mkuu anasafiri na timu kwa ajili ya mechi za Ligi Kuu kisha msaidizi wake anabaki kusima­mia mazoezi ya wale am­bao hawajasafiri na timu.

 

Ukiliweka hilo pem­beni, tayari kuna vuta nikuvute juu ya uchaguzi wao mkuu ambao mam­laka ya juu ya soka im­eshaingilia na kuchukua hatua ya kuusimamisha.

 

Shirikitisho la Soka la Tanzania (TFF) limedai kuna kanuni zimekiukwa hasa katika masuala ya ada ya fomu kwa wagombea, unajiuliza katika akili ya kawaida hao wasimamizi wa uchaguzi hawakujua kiwango cha ada sta­hiki au walifanya maku­sudi! Unajiuliza pia jinsi wagombea walivyokuwa wakisuasua kuchukua fomu kwa klabu yenye ha­dhi kubwa kama Simba!

 

Wakati hayo yakitokea kuna taarifa ambazo siyo rasmi kuwa kumekuwa na mvutano wa chinichini wa kiutawala kuhusu ucha­guzi huo, japokuwa hazina uthibitisho lakini kama kweli zipo dalili siyo nzuri.

Kwa picha ninavyoiona kipindi hiki, ikitokea timu yao ikapoteza mchezo au kushindwa kupata ush­indi huku upande wa pili yaani Yanga wakashinda, haitakuwa ajabu kuo­na kukiibuka mvutano mkubwa zaidi na wa wazi.

 

Hivyo, kuepuka yote hayo ni vema Wanasimba wenyewe wakatambua kuwa, kama ni kikosi wana­cho kizuri, usajili ulifanyika vizuri na walipata muda mzuri wa kuweka kambini hivyo upepo mchafu wa muda mfupi hautakiwi ku­wapotezea dira, watam­bue imewachukua miaka mingi kurejea kwenye mstari waliopo sasa hivi.

 

Michuano ya Afrika ili­kuwa ni ndoto kwa miaka kadhaa ya hivi karibuni, Simba watashiriki tena msimu ujao katika mi­chuano ya kimataifa, hivyo wanatakiwa kuwa na kiko­si imara ambacho ili kiwe bora ni vema uongozi wa klabu nao ukawa imara.

Vuvuzela Mawasiliano, JOHN JOSEPH

Comments are closed.