The House of Favourite Newspapers

Tite: Neymar Yupo Fiti na Atacheza Mchezo Unaofuata Mashabiki Ondoeni Shaka

0
Neymar Jr aliumia kifundo cha mguu katika mchezo dhidi ya Serbia

KOCHA Mkuu wa Timu ya Taifa ya Brazil Tite amethibitisha kuwa nyota wa timu hiyo na klabu ya Paris Saint Germain ya nchini Ufaransa Neymar Da Silva Junior ataendelea kushiriki mashindano ya fainali ya Kombe la Dunia nchini Qatar na atakuwepo katika kikosi kitakachocheza mchezo unaofuatia kwenye kundi lake.

 

Tite amelazimika kuibuka na kutoa kauli hiyo kufuatia kuwepo kwa tetesi kuwa nyita huyo anaweza asiendelee na mashindano hayo kufuatia majeraha aliyoyapata katika kifundo chake cha mguu kwenye mchezo wa kwanza hatua ya makundi dhidi ya Timu ya Taifa ya Serbia.

Kocha wa Timu ya Taifa ya Brazil, Adenor Leonardo Bacchi marufu kama Tite

“Msijari Neymar atacheza Kombe la Dunia. Ataendelea kucheza, mnaweza kuwa na uhakika na hilo. Kocha Tite aliwaambia Waandishi wa Habari.

 

Katika mchezo huo dhidi ya Serbia, Timu ya Taifa ya Brazil ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-0, mabao yote yaliwekwa kimiani na mshambuliaji wa Totenham Hotspurs Richarlison.

Leave A Reply