The House of Favourite Newspapers

USIKU WA USWAZI DAR LIVE, IDDI EL FITRI ILIKUWA NOMA AISEE!!! (PICHA +VIDEO)

Mashabiki waliojitokeza usiku wa Uswazi Dar Live kusherehekea  Siku Kuu ya Idd El Fitri

Mashabiki wa burudani haswa wapenzi wa muziki wa singeli usiku wa kuamkia leo katika kusherehekea  Siku Kuu ya Idd El Fitri walipata bonge la burudani kwenye Uwanja wa Taifa wa Burudani wa Dar live katika onesho maalum la usikuwa uswazi ambalo lilikuwa noma saaana aisee.

Dullah Makabila akiwaimbisha mashabiki.

Katika onesho hilo miamba wa singeli walionesha na umwamba katika mpambano huo ulianza kutimua vumbi baada ya kumalizika kwa michezo ya watoto.

Dullah akichagua kabila la kuoa, aiseee, we acha tu.

Katika mtifuano huo aliayeanza kurusha mawe alikuwa Mfalme Ninja ambaye baada ya kuwalimisha vyakutosha mashabiki alimpisha jukwaa, Dullah Makabila.

Snura naye aliingilia kati na kufanya bonge la balaa.
Mashabiki wakiwa katika ‘mzuksi’ wa kiuswazi.

Dullah Makabila wakati akiendelea kutafuta kabila la kuoa fungakazi ilikuwa kwa Sholo Mwamba ambaye aliwasugulisha gaga watoto wa uswazi mpaka majooo… Ama kweli Usiku wa Uswazi ulikuwa noma sana.

Vidume wakifanya yao
Mfalme Ninja

Shabiki huyu nae mmmh… kuwachanukia msamba manjemba wa ‘Darisalama’ hakuona hatari.
Mfalme wa uswazi, Selemani Jabiri a.k.a Msagasumu kama kawaida yake akifanya yake.
Ama kweli anayefunga shoo ndiye mbabe wa vita, ndivyo alivyofanya Sholo Mwamba, mshakaji aligonga shoo mpaka masela wakasema baaas.

HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS/GPL 

Comments are closed.