VILIO, simanzi na mazjonzi vimetawala miongoni mwa waombolezaji leo Jumamosi, Septemba 8, 2018 wakati wa kuaga mwili wa mwanakwaya Mariam Charles (25) anayedaiwa kuuawa na mchumbaake.
Mwili wa Mariam umeagwa kwenye ibada ya mazishi iliyofanyika katika Kanisa la African Inland lililopo Chang’ombe Jijini Dar es Salaam huku ibada ikihudhuriwa na umati mkubwa waombolezaji wakiwemo wanakwaya wenzake.
Mwanakwaya huyo ambaye alikuwa mkazi wa Keko Furniture, wilayani Temeke jijini Dar alikutwa ameuawa kwenye Gesti ya East London, Mtaa wa Kwa Hamad Bonge, Temeke, Septemba 5, mwaka huu huku mchumba wake aliyetajwa kwa jina la Frank ambaye amehusishwa na mauaji hayo.
Baada ya ibada na kuagwa, mwili huo umezikwa leo katika makaburi ya temeke.
MWANAKWAYA ALIYEUAWA GESTI, FAMILIA YASIMULIA MAZITO – VIDEO
Picha na Richard Bukos | GPL
Comments are closed.