GLOBAL TV ONLINE kupitia kipindi chake cha Michezo cha Spoti Hausi kinachoruka kila Alhamisi, saa 10:00 imewatangaza washindi wa shindano la SPOTIHAUSI-TECNO lililodhaminiwa na Kampuni ya Simu ya TECNO Mobile Limited.
Washindi hao ni miongoni mwa walioshiriki kwenye Kipindi cha SpotiHausi LIVE cha Alhamisi 8, 2018 ambao ni Omary Barak na Renatus Fidel, wanatakiwa kufika katika Ofisi za Global Group zilizopo Sinza Mori – Dar, kuchukua zawadi zao za jezi mpya za Klabu vinara wa Ligi Kuu ya Uingereza, Manchester City.
Zawadi hizo zimetolewa na Kampuni ya TECNO Mobile Limited. Kwa mawsiliano zaidi, washindi wapige simu namba 0713 479 875 ili wapewe utaratibu wa kuchukua zawadi zao.
Zawadi nyingine zitaendelea kutolewa Alhamisi hii na kila Alhamisi saa 10 kamili jioni wakati wa Kipindi cha Spoti Hausi LIVE. Endelea kufuatilia SpotiHausi uibuke mshindi wa jezi za Man City, mpira na simu ya TECNO Camon CM.
Comments are closed.