The House of Favourite Newspapers

ZAMARADI: MUME WANGU HANA JEURI YA KUNIACHA

Zamaradi Mketema

MTANGAZAJI maarufu wa Televisheni ya Clouds, Zamaradi Mketema amesema kuwa watu wengi wamekuwa wakiongea maneno ya kufanya ndoa yake iingie doa ili watengane.  Akizungumza na Za Motomoto, Zamaradi alisema kuwa kamwe mumewe huyo ambaye sasa wanakaribia miaka miwili wako pamoja hana jeuri ya kumpa talaka au kumuacha.

“Ni hivi wacha waongee tu vitu wasivyovijua lakini hayo maneno hayawezi kumfanya mume wangu aniache kwa sababu jeuri hiyo hana na wala mimi siwezi kumuacha kwa namna yoyote ile,” alisema Zamaradi.

Comments are closed.