The House of Favourite Newspapers

Zana Coulibaly Bado Yupoyupo

KAMA utani vile beki wa kupanda na kushuka ndani ya kikosi cha Simba Zana Coulibaly amerejea Bongo ambapo kwa sasa anakamilisha mazungumzo na mabosi wa Simba kwa ajili ya msimu ujao.

 

Coulibaly ambaye aliletwa kuwa mbadala wa Shomari Kapombe imeelezwa kuwa uwezo wake umemkosha Kocha Mkuu, Patrick Aussems na amependekeza asiachwe msimu ujao.

 

“Coulibaly kwa sasa anakula upepo wa Dar na tayari mazungumzo yamefika sehemu nzuri hivyo muda wowote kuanza sasa atatangazwa kuwa mali ya Simba kwa kandarasi ya miaka miwili,” kilieleza chanzo hicho.

 

USAJILI WA SIMBA: KAHATA RASMI SIMBA

Comments are closed.