The House of Favourite Newspapers

Rais wa zamani wa FIFA Joao Havelange afariki dunia

0

joao-havelange-750px_0

Aliyekuwa Rais wa zamani wa FIFA Joao Havelange enzi za uhai wake.

Rais wa zamani wa FIFA Joao Havelange amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 100. Mbrazil huyo alikuwa mtangulizi wa Sepp Blatter katika shirikisho la mpira wa miguu duniani kuanzia mwaka 1974 hadi 1998.

Alijiuzulu nafasi ya Urais wa FIFA April 2013 kufuatia uchunguzi wa madai ya kupokea rushwa, na kulazwa hospitalini mwaka uliofuata alipokumbwa na ugonjwa wa mapafu.

Alikuwa mmoja wa wanakamati wa Olympic (IOC), kuanzia mwaka 1963 hadi 2011 alipojiuzulu kwa sababu ya kudhoofu kwa afya yake.

Havelange aliiwakilisha Brazil katika mashindano ya Olympic ya Kuogelea mwaka 1936, mwaka ambao aliidhinishwa kuwa mwanasheria kabla ya kuchaguliwa na IOC.

Akiwa kiongozi wa FIFA aliongeza washiriki wa kombe la dunia kutoka timu 16 hadi 32, ambapo mashindano 6 yalifanyika chini ya utawala wake.

CHANZO: BBC SWAHILI

Hatari; Bi Harusi Aliyetekwa Siku ya Send Off Yake

Basata; Nay wa Mitego Huru Kuendelea na Muziki

Wema na Mama Yake Hii ni Zaidi ya Movi……

Masanja Mkandamizaji Avunja Mbavu Watu Kwenye Harusi Yake

Harusi ya Masanja Ilivyotikisa Jijij la Dar es Salaam………

Harusi ya Masanja Mkandamiza Ilivyoacha Stori Midomoni mwa Watu….

Leave A Reply