RAPA na Meneja wa lebel ya G.O.O.D Music, Pusha T amethibitisha kuwa album mpya ya Big Sean inaelekea kukamilika na itatolewa rasmi mwanzoni mwa mwaka 2016.
Big Sean alishika nafasi ya juu kwenye chati na albamu yake ya tatu ya Dark Sky Paradise mwaka huu.
Kwa upande wake Pusha T alisema anaprojekti ya kuitangaza albamu yake mpya ya King Push – Darkest Before Dawn iliyoshika namba 20 kwenye billboard katika wiki yake ya kwanza, projekti itayomalizika Aprili kwenye miji ya Los Angeles, Atlanta, Philadelphia, New York, Boston, and Chicago.

