
Walianza hivi.

Kocha Mayanja akionesha kwa mifano jinsi anavyotaka.

Ibrahim Ajib ‘Kadabra’ akijaribu kufuata maelekezo ya kocha.

Said Ndemla (kulia), Said Issa wakitifuana kwenye mazoezi hayo.

Hija Ugando aliyeruka na Jonas Mkude wakiwania mpira huku Novatus Lufunga akijiandaa kutoa msaada.

Wachezaji wakipiga tizi.
KIKOSI cha Simba leo kimenaswa kikiendelea na mazoezi kwenye Kambi ya JKT – Mbweni iliyopo nje kidogo ya Jiji la Dar chini ya kocha wake, Jackson Mayanja raia wa Uganda.
Kikosi hicho baada ya kutolewa kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho na Caostal Union ya Tanga kinajiwinda na mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Toto Africans ya jijni Mwanza keshokutwa Jumamosi.
(HABARI/PICHA : RICHARD BUKOS /GPL)