majaji wakifuatilia kinyang’anyiro
Mshindi wa Tarent Miss Dar City Center, 2016 Sporah Luhende akiwa kwenye pozi
HATIMAYE shindano la kumtafuta Miss Dar City Centre Talent limefanyika jana katika Ukumbi wa Maisha Basement uliopo Kijitonyama jijini Dar.
Katika kinyang’anyiro hicho, kilichoshirikisha warembo kibao hatimaye mrimbwende Sporah Luhende aliibuka mshindi wa kipaji baada ya kuimba Wimbo wa Mahaba Niue wa msanii Maua Sama.
Kilele cha shindano hilo la warembo linatarajiwa kuwa Mei 21, mwaka huu ndani ya Ukumbi wa Golden Tulip City Centre.
Shindano hilo limedhaminiwa na Kampuni ya Global Publishers kupitia Bahati Nasibu ya Shinda Nyumba inayoendeshwa kupitia Magazeti ya Championi, Ijumaa, Risasi, Amani, Uwazi ambapo droo ya ndogo ya bahati nasibu hiyo itachezeshwa Mei, 18 na droo kubwa yenye ushindi wa nyumba itachezeshwa mwezi ujao.
Na waandishi wetu/GPL
















