×

Julieth Katebe Atwaa Taji la Miss Dar City Centre 

Miss Dar City Centre (1)

Mshindi wa shindano la Miss Aqua Dar City Centre, Julieth Katebe akiwa katika pozi baada ya kutangazwa mshindi.

Miss Dar City Centre (2)
Tano Bora ya Miss Aquar Dar City Centre.

Miss Dar City Centre (3)
Kaimu wa nafasi ya Miss Aquar Dar City Center ambaye anamaliza muda wake, Sabina Thomas akiwa kwenye pozi. Katika mashindano yaliyopita aliibuka mshindi namba tatu.

Miss Dar City Centre (4)

Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva, Khaleed Mohamed ‘TID’ akikamua jukwaani katika shindano hilo.

Miss Dar City Centre (5)
Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva, Elias Barnabas ‘Barnaba Boy’ naye akifanya yake.

Miss Dar City Centre (6)
Afisa Masoko wa Global Publishers, Yohanna Mkanda akiwa red carpet na mrembo.

Miss Dar City Centre (7)
Top Ten ya Miss Dar City Centre wakiwa kwenye pozi baada ya kutangazwa.

Miss Dar City Centre (8)
Wanamitindo maarufu Bongo, Martin Kadinda na Hamisa Mobeto wakiwa kwenye pozi katika tamasha hilo.

Miss Dar City Centre (9)
Top 5 ya Miss Dar City Centre wakiwa kwenye pozi.

Miss Dar City Centre (10)
Warembo wakiwa kwenye red carpet na Miss Aquar Dar City Centre.

Stori: Boniphace Ngumije

Usiku wa kuamkia leo palikuwa hapatoshi ndani ya Ukumbi wa Mtana (Jengo la LAPF), Kijitonyama jijini Dar, kulimofanyikia shindano kubwa la warembo lililojulikana kwa jina la Zan Aqua Miss Dar City Centre.

Katika shindano hilo ambalo lilikuwa linadhaminiwa na Bahati Nasibu ya Shinda Nyumba inayoendeshwa na Global Publishers, kulifanyika pia burudani mbalimbali kutoka kwa wasanii Khalid Mohamed ‘TID’ na Elias Barnabas ‘Barnaba’ lakini pia watu waliohudhuria shindano hilo waliburudika kwa vinywaji na muziki mzuri.

“Shindano limekwenda vizuri, mshindi wetu Julieth Katebe amejinyakulia zawadi ya shilingi milioni moja taslimu na nywele bandia zenye thamani ya shilingi milioni moja kutoka katika kampuni ya Prima Afro, washindi wengine wamebeba zawadi mbalimbali lakini pia mshindi wa kwanza mpaka wa tano wameingia kwenye kinyang’anyiro cha Miss Ilala,” alisema mratibu wa shindano hilo, Nancy Joseph.

Leave a Comment