Msomaji wa Gazeti la Ijumaa (kushoto) akinunua kwa muuzaji wa magazeti ya Global, Hadija Rashid.
Msomaji wa Ijumaa akinunua gazeti kwa muuzaji wa magazeti ya Global.
Wasomaji wa Gazeti la Ijumaa wakinunua gazeti hilo kwa muuzaji Hadija Rashid (wa pili kulia). Anayeshuhudia kulia ni Ofisa Masoko wa Global Yohana Mkanda.
Mwanadada akinunua gazeti la Ijumaa kwa muuzaji.
Hadija (kulia) akiwauzia gazeti la Ijumaa wa eneo la Vingunguti Dar.
Wadau wa Gazeti la Ijumaa wakinunua gazeti hilo kwa bei ya Sh.1000.
Wapenzi wasomaji wa gazeti la Ijumaa, Proscovia Lasway (kushoto) na Prediganda Lasway (katikati) wakilisoma Gazeti la Ijumaa baada ya kukutwa na muuzaji wa magazeti ya Global, Hadija Rashid na kupiga nao picha.
Msomaji wa Ijumaa aliyekutwa akilisoma gazeti hilo aitwaye mama Brian, mkazi wa Kitunda jijini Dar.
Msomaji wa Gazeti la Ijumaa aliyejitambulisha kwa jina la Pasha Wali akinunua gazeti hilo kwa bei ya sh.1000.
WASOMAJI mbalimbali wa Jiji la Dar wamezidi kulifurahia gazeti la Ijumaa lenye muonekano mpya linalotoka mtaani kila siku ya Ijumaa.
Kamera yetu leo iliwafikia wakazi wa Kitunda, nje kidogo ya Jiji la Dar ambapo iliwashuhudia wasomaji mbalimbali wakijitokeza kwenye gari la matangazo la gazeti hilo na kulichangamkia kulinunua.
Akizungumza na wakazi eneo hilo, Ofisa Masoko wa Kampuni ya Global Publishers inayozalisha gazeti hilo pamoja na Ijumaa Wikienda, Uwazi, Risasi, Amani na Championi, Yohana Mkanda, alisema anawaomba wasomaji wa magazeti hayo ya Global kuendela kulinunua Ijumaa kwa bei ya Sh.1000 kwani limesheheni habari nyingi za burudani, hadithi, machombezo na mikasa.
“Magazeti yote ya Global yanauzwa kwa shilingi 500 isipokuwa Ijumaa pekee lenye muonekano mpya ndilo linauzwa shilingi 1000. Niwasihi wasomaji wetu waendelee kununua magazeti yetu ili wazidi kuhabarika, kuelimika na kuburudika,” alisema Mkanda.
NA DENIS MTIMA/GPL