×

Iyanya akumbana na kashfa ya kutolipa bili ya hoteli

iyanayya

Lagos, Nigeria

STAA wa muziki nchini Nigeria, Iyanya amekumbata na kashfa ya kudaiwa ‘kufulia’ kiasi hadi kufikia kiasi cha kutokuwa na pesa ya kulipia bili yake hotelini wakati akiwa kwenye tour ya shoo yake nchini Marekani hivi karibuni.

do moePromota Don De Moe

Kashfa hizo zimetolewa hivi karibuni na mwandaaji wa matamasha maarufu nchini  humo,  Promota Don De Moe baada ya kuufahamisha ulimwengu kupitia mtandao wa Instagram kuwa staa huyo hana chochote kwa sasa kwani hata bili anayodaiwa na hoteli ya Hilton ameshindwa kulipa, jambo ambalo limemdharirisha Iyanya.

Iyanya-billDon De Moe alisema “Iyanya, nakuomba ulipe bili yako unayodaiwa kwenye hoteli ya Hilton,” Moe aliongeza tena kuwa, “Hujalipa bili yako tangu Jumatatu, Julai 4th na nimechoka ‘kukubeba’ (kukusaidia).”

Baadaye Iyanya naye akajibu “Watu wenye chuki chuki (maadui) wanataka kumfanya mtu mwema aonekane mbaya.”

Francis, Iyanya Maneno hayo yaliwadhihirishia mashabiki wa Iyanya sata wa Kukere kuwa hajafirisika kiasi cha kushindw akulipa bili ila yawezekana kuna kutofautiana kati yake na Don De Moe.

IMG_0962Tangu atangaze kuihama lebo ya MMMG (Made Men Music Group) na kuyanzishga lebo yake mwenyewe, mambo mengi yamekuwa yakiandikwa kuhusu Iyanya aliyebamba na wimbo wa “Oreo huku akizungumzwa vibaya hususan watu aliyokuwa akifanaya nao kazi kwenye lebo hiyo.

MMMG pia ina wasanii kama Tekno, Selebobo, Mr Chibbz, na Tonye Garrick.

Leave a Comment