×

Penny aumia shisha kuzuiwa

pennyStori: Imelda Mtema

MTANGAZAJI maarufu Bongo, Penniel Mungilwa ‘Penny’ amesema kuwa ameumizwa sana na kupigwa marufuku uvutaji wa sigara aina ya Shisha, amri iliyotolewa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwani ni kitu ambacho alikuwa ‘anakizimia’ sana.

Mrembo huyo ambaye yumo kwenye listi ya wasanii waliowahi kuwa wapenzi wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, alisema Shisha ni ulevi f’lani ‘amazing’  ambao unamfanya mtu ajisikie vizuri hata kama ana msongo wa mawazo.

“Daah nimeumia sana lakini kwa sababu ni amri iliyotolewa na kiongozi mkubwa wa nchi lazima tuifuate ila nataka kujua kama hata nyumbani tunakatazwa kuitumia,” alisema Penny.

Shisha imepigwa stop na serikali kutokana kuwa na madhara kiafya kwani huweza kusababisha kansa ya mapafu.

Leave a Comment