×

JPM Amuapisha Mama Anna Mghwira Kuwa RC wa Kilimanjaro na Kumkabidhi Ilani ya CCM

Rais Dkt Magufuli akimuapisha mama Anna Elisha Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Ikulu jijini Dar es salaam Juni 6, 2017.

IKULU, DAR: Rais Magufuli amemuapisha Mwenyekiti wa ACT Wazalendo, Bi. Anna Elisha Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, leo Juni 6, 2017 na kumkabidhi Ilani ya CCM.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Tanzania Bara) Ndg. Rodrick Mpogolo akimkabidhi ilani ya CCM Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Elisha Mghwira.

Baada ya kumuapisha, Rais Magefuli alipata nafasi ya kumzungumzia RC huyo mpya.

“Mimi huwa siteui watu hivi hivi, naangalia uwezo wa mtu, wewe nimekuchunguza na nimejiridhisha kuwa una uwezo wa kuwatumikia wananchi.”

“Mimi nampongeza sana Mama Anna, ni mstaarabu, msomi mzuri na najua kwa nafasi niliyomteua atafanya kazi vizuri,” amesema Rais Magufuli.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Elisha Mgwira akisoma hati ya kiapo cha maadili ya utumishi wa umma mara baada ya kuapishwa Ikulu, Dar.

 

Baada ya kuapishwa Mghwira amesema;

“Ninasema hii ni heshima kwa Taifa letu, ni heshima kwa umoja wa nchi yetu, ni heshima kwa siasa za umoja wa nchi yetu.

“Kumekuwa na minong’ono mingi sana kuwa Rais analeta nini, kuteua watu wanaitwa wapinzani, mimi sio mpinzani wa maendeleo.

Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro, Anna Elisha Mgwira akiongea jambo la shukrani mara baada ya kuapishwa na Rais Magufuli kushika wadhifa huo.

 

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira akiingia kwenye gari lake kuelekea kituo chake cha kazi baada ya kuapishwa leo na Rais Magufuli.

VIDEO: Anna Mghwira Aukana ‘Upinzani’… JPM Awajibu Wanaosema Alikataa Kuteua Wapinzani

1 Comment

Leave a Comment